Saturday, June 30, 2012



MISS REDD'S IRINGA NI AIBU TUPU , CHIFU JAJI AZOMEWA UKUMBINI

Huyu ndie Naomi James ambaye ametawazwa usiku huu kuwa Miss Redd's mkoa wa Iringa na kuzawadiwa kitita cha shilingi 500,000
Mshindi wa taji la Miss REdd's 2012 mkoa wa Iringa Naomi James kati kati akiwa na mshindi wa pili Sarah Utiku na Catherine Mfupi ambaye ni mshindi wa tatu mara baada ya kutangazwa usiku huu ndani ya ukumbi wa Highlands mjini Iringa
Msaidizi wa chifu jaji msomi Saimon Belenge akiokoa jahazi lisizame baada ya wadau wapenzi na mashabiki wa onyesho hilo kuanza kumzomea chifu jaji Bw Tasha Jimi ambaye ni mratibu wa Miss Redd's mikoa ya kusini baada ya kuchemka kutaja namba ya mshindi wa pili katika onyesho hilo
Hawa ndio waliopenya nafasi ya tano bora kati ya washiriki 12 waliopanda jukwani wa kwanza kushoto ni Amisa Zuber, SArah Utiku, Naomi James ,Winfreda Felix na Catherine Mfupi
Wadau wa urembo leo wakiwa wamevalia nguo za heshima kiasi
Warembo wakiwa katika picha ya pamoja na washindi na washiriki wa onyesho hilo
Mgeni rasimi Naibu meya wa Manispaa ya Iringa Gervas Ndaki ( wa pili kushoto) akiwa na afisa michezo na utamaduni Manispaa ya Iringa Bw.Kadinde na mratibu wa onyesho hilo Bw Dosi
Hawa ndio majaji wa onyesho hilo katikati ni Tasha Jimbo aliyetaka kuvuruga onyesho dakika za mwisho
Msomi Saimon Belege (kulia) akicheka baada ya chifu jaji kushoto TashaJimy kuvuruga kazi yao
Madau Saimon Belege akiwa na mshindi wa taji la Miss Iringa mwaka jana na mshindi wa leo katika shindano ya Redd's Miss Iringa Naomi James


Huyu ndiye Tasha Jimy aliyezomewa kwa kushindwa kujua tofauti kati ya namba 4 na mbili hivyo kujikuta akizomewa ukumbini.




WAZIRI WA HABARI,MICHEZO,VIJANA NA UTUAMADUNI DR. MUKANGARA APATA AJALI MBAYA TABORA.

Waziri wa Habari, Michezo na Utamaduni Dokta FENELLA MUKANGARA(pichani) amepata ajali ya gari katika Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora akiwa njiani kwenda Mkoani Mwanza kikazi.

Habari kutoka Wilayani Nzega zinasema kwamba ajali hiyo imetokea leo asubuhi wakati Waziri huyo akiwa njiani akitokea Dodoma kwenda Mkoani Mwanza kuzindua Mashindano ya Vishale.
Mashuhuda wa ajali hiyo wamesema kwamba gari aliyokuwa amepanda Waziri MUKANGARA akiwa na Msaidizi wake imepinduka mara Tatu na inadaiwa kuwa Waziri huyo ameumia Mguu wa kushoto na amekimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Nzega kwa ajili ya matibabu zaidi.

No comments:

Post a Comment