Saturday, June 30, 2012



WAKATI madaktari wa hospitali za serikali nchini wameweka ngumu kutibu wagonjwa wakidai kuboreshewa mishahara, baadhi ya waganga wa kienyeji wameonekana kufurahia kwa sababu sasa wanapata wagonjwa wengi wanaotaka tiba kwao.


 
Mwenyekiti wa Chawatiata mkoa wa Iringa Bi, Christina Mgongolwa

Waganga wa jadi wametakiwa kutoa huduma bora na kwa umakini zaidi ili kulinda afya za wagonjwa wao pamoja na zao pia.

Hayo yamesemwa na katibu wa kamati tendaji ya mkoa wa Iringa dkt Maiko Evaristo Kalinga katika semina ya waganga wa jadi na wakunga iliyofanyika ukumbi wa Siasa ni Kilimo manispaa ya Iringa. Waganga hao wametakiwa kutumia njia za kisasa kama uuvaaji wa glovu ili kuzuia maambukizi ya magonjwa, pia kuboresha maeneo yao ya kazi ikiwa ni pamoja na kuwa wasafi.

Pia amewataka waganga hao kutoa tiba na kuacha kupiga lamli kwani ni chanzo cha ugomvi na mauji katika jamii.

Akiendelea kutoa mafunzo hayo amewataka watendaji wa kata na vijiji ambao wamekuwa wakiwapokea waganga wa jadi bila utaratibu maalum kuacha tabia hiyo. Kwani wamekuwa wakiwapokea waganga  ambao ni matapeli.

Pia ametoa onyo kwa wakunga wa jadi kuwa hawaruhusiwi kutoa dawa za asili kwa kina mama wajawazito kwani wamekuwa wakichangia kwa kiasi kikubwa vifo vya watoto wachanga na kina mama, badala yake wametakiwa kutoa ushari kwa wajawazito kuhudhuria hospitali.


Naye mratibu wa waganga wa jadi mkoa wa iringa Ibrahim Kamisa amewasomea masharti ambayo serikali kupitia wizara ya afya na ustawi wa jamii wameweka sheria kwa waganga  hao wa jadi.

Semina hiyo iliambatana na ugawaji wa lesini kwa waganga 19 wa jadi ambao wamekwisha sajiliwa. Akigawa leseni hizo mkuu wa wilaya  dokta Leticia Warioba amesema kuwa waganga hao wanatakiwa kushirikiana katika shughuli zao, wawe wasafi na kutoa ushauri kwa wagonjwa waende hospitali mapema pale wanaposhindwa kuwatibia.

Pia amewapongeza waganga waliopewa leseni na kutoa wito kwa waganga ambao hawajasajiliwa  kujisajili mapema ili nao waweze kupewa leseni

No comments:

Post a Comment