Tuesday, June 4, 2013

WADAU WAKISHIRIKIANA KWA PAMOJA UJANGILI WA MENO YA TEMBO UTAKOMA

Naibu Waziri wa mali asili na utalii, Lazaro Nyalandu akifungua kikao cha wadau wa ulinzi wa mali asili juu ya janga la ujangili wa tembo mikoa ya Nyanda za juu kusini kinachofanyika kwenye ukumbi wa siasa ni kilimo Manispaa ya Iringa. Kikao hicho kimejumuisha viongozi waandamizi wa serikali katika mikoa mitano, Taasisi za kimataifa ikiwemo INTERPOL

Wadau wa mazingira na udhibiti wa meno ya Tembo nyanda za juu kusini



Wadau wa sekta ya maliasili na utalii mikoa ya nyanda za juu za juu kusini wametakiwa kushiriki ipasavyo katika jitihada za pamoja katika kukabiliana na tatizo la majangili wa wanyama katika maeneo yanayopakana na hifadhi za taifa.
Maadhimio hayo yametolewa katika semina ya wadau wa ulinzi wa maliasili juu ya wimbi la ujangili wa tembo nyanda za juu kusini baada ya wadau hao kuonesha nia ya pamoja katika kuhakikisha wanapambana kwa kushirikiana na vyombo vya usalama katika maeneo hayo kudhibiti vitendo hivyo ambapo kila mwaka zaidi ya tembo elfu 10 huuwa.

Semina hiyo iliyoandaliwa na mradi wa kuboresha usimamizi  na uhifadhi wa mazingira, Strengthening the Protected Area Network in Southern Tanzania SPANSET imelenga kujadili jitihada za makusudi za wadau hao wakiwemo ofisi za wakuu wa mikoa Iringa,Mbeya,Njombe na Dodoma pamoja na asasi mbalimbali zikiwemo Interpol Tanzania,Interpol Kenya,Cites/Mike Tanzania,Trafic Tanzania na wadau wengine wa maliasili na utalii ambao wanalenga kukabiliana na tatizo hilo la ujangili wa wanyama hususani tembo.

Katika semina hiyo imebaini kuwepo kwa changamoto nyingi zinazo ikabili sekta ya maliasili na utalii hapa nchini na kuathiri kwa kiasi kikubwa Rasilimali wanyama ambapo baadhi ya changamoto hizo ni pamoja na kuwepo kwa kundi kubwa la wahamiaji haramu katika misitu iliyo karibu na mbuga,kuzagaa kwa silaha zinazoletwa na wageni kutoka nchi za jirani ambazo zina migogoro ya kisiasa,kukua na kuongezeka kwa shughuli za kibinadamu hususani kilimo pamoja na kushamili kwa biashara haramu ya nyara za serikali  zikiwemo meno ya tembo,pembe za faru pamoja na ngozi za wanyama mbalimbali.

Hivyo wadau hao wameishauri serikali pamoja na wananchi kushirikiana kwa pamoja katika kutoa taarifa katika vyombo vinavyohusika pindi wanapoona matukio ya kijangili yanajitokeza kwani wanao husika na vitendo hivyo wapo katika jamii.

Kwa upande wake profesa Mutayoba wa chuo kikuu SUA mkoani morogoro ambaye ndiye mmoja wa watafiti wa DNA nchini ameshauri kutumia vipimo kupima pembe hizo kitaalamu ilikubaini mahali zinapotoka ili kuongeza udhibi

No comments:

Post a Comment