Tuesday, March 11, 2014

MASHINE ZA KUTOLEA LISITI (EFDs) KAZI BADO IRINGA WATAKIWA KUTEKELEZA AGIZO LA SERIKALI
[Image]
Meneja wa Mamlaka ya Mapato (TRA) mkoa wa Iringa, Rosalia Mwenda akizungumza na mtandao huu
Wafanyabiashara mkoani iringa wametakiwa kutumia elimu wanayoipata kupitia semina mbalimbali zinazotolewa na mamlaka ya mapato Tanzania TRA ili waweze kufaham zaidi matakwa ya sheria.
Rai hiyo imetolewa na meneja wa mamlaka hiyo mkoani Iringa Bi Rosali mwenda wakati akizungumza na Overcomers redio ofisini kwake hii leo  kuhusiana na mwenendo mzima wa utumiaji wa mashine za kielectronic kwaajili ya kutolea lisiti kwa wateja (EFDs)
ambapo amesema kuwa zoezi hilo linaendelea kuwepo kwa mujibu wa sheria kwani hakuna mtu wala kikundi cha watu walioamua kuwepo kwa mashine hizo bali ni uamuzi wa serikali ili kudhibiti na kurahisisha ukusaji wa mapato nchini.
Hivyo amewataka wafanyabiashara mkoani hapa kutambua kuwa suala la kutumia mashine hizo ni la kisheria pia wanatakiwa kulichukulia uzito kwani kupuuzia zoezi hilo ni ukiukwaji wa sheria iliyowekwa na mamlaka husika.
Aidha Bi Mwenda amesema wafanyabiashara watambue kuwa awamu ya kwanza ya utumiaji wa mashine hizo umekamilika uliokuwa ukiwahusisha wale walio na mtaji wa kuanzia zaidi ya  million 40  na sasa wameanza awamu nyingine inayohusisha wale wenye mtaji wa kuanzia milioni 14 hadi 39 na itaendelea hadi itakapofika kwa wafanyabiashara wote.
Akielezea juu ya mahusiano ya mamlaka hiyo na wafanyabiashara Bi Mwenda amesema kwasasa hakuna tatizo lolote kati yao na mpaka sasa wameanza kuwapelekea barua za kuwakumbusha wafanyabiashara wanaotakiwa kuwa na mashine hizo.
Ajali yaua Mmoja Iringa

Mtu mmoja ameripotiwa kufariki dunia mkoani Iringa kwa ajali ya gari.
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Iringa Ramadhan Mungi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema kuwa ajali hiyo imelihusisha gari dogo aina ya Toyota Noah lenye namba za usajili T 142 CRA lililokuwa likitokea Iringa kuelekea Dodoma.
Kamanda Mungi amesema ajali hiyo imetokea mnamo tarehe 10.03.2014 majira ya saa 11:00 jiaoni katika eneo la Igingilanyi wilaya ya Iringa vijijini  ambapo amemtaja dereva wa Gari hilo kuwa ni Darton Ilomo(22) mwanafunzi wa Chuo cha UCC Kilichopo jijini Dar es salam
Aidha amemtaja aliyefariki kutokana na ajali hiyo kuwa ni Rose Mwakabuku (55) muuguzi katika hospitali ya mkoa wa Iringa ambaye pia ni mkazi wa mwembetogwa katika manispaa ya Iringa mjini na amesema marehemu amefariki akiwa anapatiwa matibabu katika hospital ya mkoa wa Iringa, huku chanzo cha ajali hiyo kikiripotiwa kuwa ni mwandokasi hivyo Mungi amewataka madereva kuwa wastaarabu pindi wanapoendesha vyombo vya moto.
 

No comments:

Post a Comment