WANANCHI IRINGA WAILILIA IRUWASA
Wananchi katika manispa ya
Iringa wameiomba idara ya maji(IRUWASA) mkoani
hapa kuboresha miundombinu ya maji iliyoharibika na kusababisha uvujaji wa maji
kiholela katika maeneo mengi ya manispaa hiyo.
Wakizungumza na Mtandao huu wananchi hao wameonesha kusikitishwa kwao na tatizo la uvujaji wa maji
kiholela jambo ambalo limekuwa likisababisha kukosekana kwa huduma hiyo katika
maeneo yao ambapo wameyataja maeneo yaliyo athiriwa na uvujaji wa maji hayo
kuwa nia pamoja na Mlandege,Flelimo,Mwangata na maeneo ya mshindo.
Wamesema kuwa kutokana na
uvujaji huo unachangi kwa kiasi kikubwa katika uharibifu wa miundo mbinu kama barabara na maeneo ya makazi ya watu hivyo wameuomba
uongozi wa idara hiyo kulishughulikia ili kupunguza kero hiyo.
Kwa upande wake afisa
mahusiano wa idara ya maji manispaa ya iringa bi Restuta Sakila alipohojiwa na mtandao huu ili kulizungumzia tatizo hilo
amekili kuwepo kwa tatizo hilo ambalo amesema
tayari wameiweka mikakati maalum kwaajili ya kurekebisha tatizo hilo,ambapo mpango huo
utaanza kushughulikiwa mapema mwezi huu kwa kuwa tayari kila kitu kipo tayari
Hivyo amewaomba wananchi
kutoa ushirikiano wa karibu na idara hiyo pale wanapoona tatizo ambalo ni kubwa
kutoa taarifa ili liweze kushughulikiwa mapema iwezekanavyo kupunguza uharibifu
huo.Pia amewataka wananchi kuto watumia mafundi wanaochangisha fedha za
matengezo nje ya ofisi ili kupunguza kero hizo.
No comments:
Post a Comment