Tuesday, February 21, 2012

FEBRUARY 21/2012

Chama cha watu wenye ulemavu manispaa ya Iringa mjini, kimeyataka mashirika binafsi yanayoomba miradi ya kusaidia watu wasiojiweza kupitia barua za maombi yao na kuhakikisha wanatekeleza yale waliyo yaandika katika barua hizo.

Akizungumza na mtandao, katibu wa chama hicho manispaa ya Iringa bwana Haruna Mbata amesema tayari wamebaini kuwa kuna baadhi ya mashirika ambayo yaliomba yapewe fedha za kuwasaidia watu wasio jiweza wakiwemo wajane,walemavu,watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu baada ya kupokea fedha hizo matokeo yake hujinufaisha wenyewe.

Aidha bwana mbata amesema, kutoka na vitendo vinavyofanywa na baadhi ya mashirika hayo ya kutotekeleza majukumu yao kimewafanya waweze kutengeza mikakati maalum kwaajili ya kukagua nyaraka zote zilizoandikwa ili kuona ikiwa wanatekeleza ipasavyo, pindi itakapobainika kuwa kuna ubadhirifu ifikapo mwezi wa kumi na mbili mwaka huu, amesema  watatakiwa kufuta yale waliyoyaandika katika miongozo hiyo.

Hivyo amewataka wale wanaosimamia miradi hiyo kutekeleza yale waliyoyandika kwa kuwasaidia watu wasiojiweza kuliko kujinufaisha wenyewe kwani kufanya hivyo nikosa kwamujibu wa usajili wa miradi hiyo



FEBRUARY 21/2012

S

No comments:

Post a Comment