Ziara ya Mbunge wa njombe Magharibi
zawafurahisha wananchi wa jimbo lake.
Naibu waziri wa maji ambaye pia ni mbunge wa jimbo la
Njombe Magharibi Mhandisi Gerson Lwenge ameanza ziara ya siku nane kuwatembelea
wananchi wa jimbo lake huku akieleza mambo mbalimbali pamoja na kuchangia
maafa yanayo likumba jimbo hilo.
Katika ziara hiyo jana Waziri Lwenge ameanzia
katika kata ya Igima kwa kuanza na kitongoji cha mawindi ambako
ametoa shilingi laki tatu ili kuanzishia mfuko wa maafa ya kijiji ikiwa
ni zoezi la kuanzisha mifuko hiyo kwa kila kijiji jimboni humo.
Jumla ya nyumba Tatu zilikumbwa na maafa hayo kufuatia
kunyesha kwa mvua kubwa zilizoambatana na upepo mkali februari 11 mwaka
huu na kusababisha hasara kubwa katika nyumba hizo zinazogharimu
takribani milioni mbili ukarabati wake.
Akisoma taarifa ya kijiji cha Igima mwalimu mkuu wa
shule ya Msingi Igima mwl.Cremence Mwalongo amesema kuwa licha ya mafanikio
mbalimbali yaliyopo kijijini hapo lakini pia kijiji kinakabiliwa na changamoto
mbalimbali zikiwemo za kielimu.
Baadhi ya changamoto zilizobainishwa kwenye Risala
hiyo ni pamoja na ukosefu wa vifaa mbalimbali katika shule ya sekondari ya
Igima hali iliyopelekea shule hiyo kushindwa kufanikisha hata mwanafunzi mmoja
kujiunga na kidato cha tano mwaka huu kati ya wanafunzi 121.
Kufuatia changamoto hizo pia mhandisi Lwenge hakusiti
kutumia fursa hiyo kuwataka wananchi wa kijiji hicho kuachana na itikadi za
kisiasa kwa kipindi hiki badala ya kujikita katika shughuli za kimaendeleo.
Ziara hiyo kwa siku ya leo inaendele katika kata ya
Ulembwe ikianzia kijiji cha Ulembwe huku ikimalizika katika kijiji cha Usalule
ukiwa ni muendelezo wa ziara yake ya juma zima.
No comments:
Post a Comment