Polisi jamii Iringa kupewa kipaombele ili kutokomeza uharifu
Wananchi mkoani Iringa
wameaswa kutoa ushirikiano wa karibu kwa jeshi la polisi ili kutokomeza uharifu
katika jamii.
Rai hiyo imetolewa na
Afisa mnajimu wa jeshi la polisi mkoani hapa bwana Bundara Musiba wakati wa
mahojiano maalum na mtandao huu juu ya njia za kutokomeza uharifu pamoja na
Polisi jamii katika mkoa wa Iringa ambapo amesema wananchi wanao wajibu wa
kuhakikisha wanatoa taarifa ya uharifu pindi unapo jitokeza katika maeneo yao.
Amesema suala la
polisi jamii ni la msingi kwani linaweza kusaidia jeshi la polisi kutambua maeneo
ambayo kunatokea uharifu pia kuwatambua watu wanaojihusisha na vitendo vya
uharifu,hii imekuja kutokana na matukio ambayo yamekuwa yakijitokeza mara kwa
mara katika mkoa wa iringa yakiwemo ya watu kujinyonga na pia kuuawa kwani
kuliachia jeshi la polisi pekee haliwezi bali wanahitaji nguvu zaidi kutoka kwa
wananchi kwani ndiyo wanaoishi karibu na waharifu hao.
Aidha ameshauri jamii
kuacha vitendo vya kuchukua sheria mkononi pindi wanapo mkamata muharifu na
badala yake wamfikishe katika kituo cha polisi kwani kufanya hivyo kunaweza
kusaidia jeshi la polisi kuwakamata waharifu wengine baada ya mahojiano na
mtuhumiwa kwani anaweza kuwataja waharifu walio shirikiana katika kufanya
uharifu.
No comments:
Post a Comment