Tuesday, June 5, 2012

Mhanga wa tukio la ajali ya moto Bi  Jojina Kahemela akitahamaki kilicho sababisha kuunguliwa na nyumba
Mwenyekiti wa mtaa wa Frelimo C Bwana Geoge Mwanjombe akishuhudia tukio
Hii ni nyumba iliyoathiriwa na ajali ya moto ikionekana kwa nje imeathiriwa ndani
Wananchi wa Frelimo C wakisaidia kuokoa mali zilizo nusulika wakati wa tukio
Baadhi ya wakazi wa Frelimo C wakishuhudia ajali ya moto ilivyotokea
Mwandishi IMTV Ibrahim Kitan'gara akishuhudia tukio la moto
Baadhi ya vyombo vilivyo nusulika katika ajili ya moto na kuokolewa na wasamlia wema wa mtaa wa frelimo



                Gari ya zima moto ikisaidia kuzima moto katika mtaa wa frelimo                     
Nyumba moja katika mtaa wa Frelimo C kata ya kwakilosa manispaa ya Iringa mjini imenusurika kuteketea baada ya kutokea kwa hitlafu ya umeme na kusababisha moto ulio unguza baadhi ya mali za nyumba hiyo.

Ajali hiyo imetokea majira ya saa moja na nusu za asubuhi hali ambayo imewashangaza wengi hususani wananchi wa maeneo hayo walioshiriki kuokoa baadhi ya mali zilizokuwemo katika nyumba hiyo na jitihada hizo kuweza kuzaa matunda na kufanikiwa kuzima moto huo.

Akizungumzia juu ya ajali hiyo mmiliki wa nyumba hiyo Bi Jojina Kahemela amesema chanzo cha moto huo ni shoti ya umeme iliyojitokeza ambayo imeanzia katika chumba chake ambako ndiko walilala watoto japo anasema anashindwa kutambu chanzo cha hitlafu hiyo,hivyo amewaomba wananchi wenye mapenzi mema kumsaidia baadhi ya vitu vilivyo haribiwa na moto huo ikiwemo magodoro,vyombo mbalimbali pia amewashukuru wananchi waliojitokeza kumsaidia kuzima moto huo bila nguvu ya zima moto ya manispaa ambao waliwasili katika tukio hilo na kukuta hali imetulia.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mtaa huo Bw Geoge Mwanjombe amewapongeza wananchi wa mtaa wake kwa ushirikiano walio uonesha katika kusaidia kuzima moto huo ambao usinge shughulikiwa mapema ungeweza ksababisha madha makubwa zaidi nao mashuda wa tukio hilo wamezungumzia tukio hilo kuwa limewashtua lakini wametoa tahadhari kwa jamii kuwa makini na matumizi ya umeme ili kuepusha matukio ya ajali yatokanayo na umeme.   

No comments:

Post a Comment