Saturday, August 18, 2012

 Kaya 55 zilizopo Wilayani Magu, mkoa wa Mwanza hazina mahali pa kuishi baada ya nyumba zao zaidi ya 90 kubomolewa kisha kuchomwa ikiwa ni sehemu ya kutimiza amri ya Serikali nyumba hizo kubomolewa kupisha eneo hilo linalotajwa kuwa ni Hifadhi ya Taifa.

Tukio hilo linadaiwa kufanyika kuanzia tarehe 1 Agosti hadi Agosti 2 mwaka huu, ambapo zoezi hilo liliendeshwa chini ya usimamizi wa Mkuu Mpya wa wilaya hiyo Jacquline Liana, akishirikiana na Jeshi la  polisi Wilayani humo.

No comments:

Post a Comment