JK:Aahidi Kifuta Jasho Cha Ng'ombe 1500 Kwa Wananchi Wa Wilaya Tatu Za Mkoa Wa Arusha
SERIKALI
itakuwa inagawa ng’ombe 1500 kila mwezi kwa wananchi wa wilaya tatu za
Mkoa wa Arusha kama kifuta jasho cha kupoteza kiasi cha karibu mifugo
800,000 iliyopotea kutokana na ukame na athari zake mwaka 2008/2009.
Ahadi hiyo imetolewa leo, Alhamisi, Agosti 2,
2012 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya
Mrisho Kikwete wakati alipozindua Mradi wa Serikali wa Uwezeshaji Mifugo
kwa waliopotelewa mifugo yote katika Wilaya ya Monduli kwenye sherehe
iliyofanyika Makuyuni wilayani humo.
Katika uzinduzi huo uliohudhuriwa na viongozi
wa Mkoa wa Arusha wakiwemo wakuu wa wilaya na wabunge wa mkoa huo, Rais
Kikwete amegawa ng’ombe 500 kwa kundi la kwanza la wananchi ikiwa ni
mitamba minne na dume moja la kisasa kwa kaya 16 za mwanzo.
Uzinduzi huo ni wa pili kufanywa na Rais
Kikwete chini ya Mradi huo wa kwanza wa aina yake kubuniwa na Serikali
katika historia na wenye thamani ya sh. Bilioni 12.9.
Februari 19, mwaka huu, Rais Kikwete
alizindua Mradi kama huo katika Wilaya ya Loliondo kwenye sherehe
zilizofanyika mjini Loliondo. Kesho Agosti 3, 2012 Rais Kikwete
anatarajiwa kuendelea na zoezi hilo katika mji wa Loliondo
DK KIGODA AITAKA TBS KUFANYA UKAGUZI WA BIDHAA KUTOKA NJE YA NCHI
WAZIRI
wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda amelitaka Shirika la Viwango
(TBS),
kuhakikisha linafanya ukaguzi wa bidhaa kutoka nje kabla hazijaingizwa
nchini
ili kuepukana na tabia nchi hii kugeuzwa dampo la bidhaa hafifu.
Kauli
hiyo aliitoa jijini Dar es Salaam jana, wakati alipokuwa akizindua Ofisi
ndogo
ya shirika hilo, inayoshughulika na ukaguzi wa bidhaa zinazotoka nje ya
nchi.
Dk
Kigoda alisema iwapo shirika hilo litafanikiwa kudhibiti uingizwaji wa
bidhaa
hafifu nchini anaamini kelele zote zinazopigwa kuwa wao ndio chanzo cha
uingizwaji wa biadhaa hizo zitakwisha.
“Nawaagiza
TBS kupitia madukani na sokoni ili kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa
ubora wa
bidhaa na zile bidhaa mtakazokuta ni hafifu, zitoweni na kuziharibu na
hao
wafanyabishara watozwe faini za kuharibu bidhaa zao”alisema Dk Kigoda.
Alibainisha
kuwa Wizara yake inatarajia kupata taarifa juu ya utekelezaji wa maagizo
hayo
kwa vipindi vya kila robo mwaka ili kujua utaratibu wa utekelezaji.
Akifafanua
madhumuni ya wizara ni kushirikiana na taasisi nyingine za serikali kama
vile
Mamlaka ya Mapato (TRA) Baraza
la Mazingira ,Mamlaka ya Chakula na Madawa (TFDA), Mkemia Mkuu wa
serikali, pamoja na Tume ya Ushindani ili kuhakikisha bidhaa za nje
zinapimwa
maridhawa.
“Ili
shehena za bidhaa hafifu zizibitiwe kuingia sokoni na kurudishwa
zilikotoka”
kwa mujibu Dk Kigoda.
Naye
Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi
ya shirika hilo, Oliver Mhaiki alitabanaisha kwamba uzinduzi wa ofisi
hiyo ni
muendelezo wa jitihada za shirika kusogeza huduma kwa wateja.
Vile
vile alifafanua kuwa TBS
imeshapanua wigo kwa kufungua ofisi katika maeneo mbalimbali kama vile
Sirari, Holili, Horohoro, Bandari ya Tanga sanjari na Namanga mkoani
Arusha,
kwa lengo la kuwasogezea huduma wadau na kuwapunguzia adha katiaka
shughuli zao
za kibiashara.
RAMBIRAMBI MSIBA WA MSAFIRI MKEREMI
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko taarifa za
kifo cha mwamuzi wa zamani wa kimataifa Msafiri Mkeremi kilichotokea leo
alfajiri (Agosti 2 mwaka huu) kwenye Hospitali ya Wilaya ya Urambo
mkoani Tabora.
Licha
ya kuwa mwamuzi, Mkeremi aliwahi kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya
Chama cha Mpira wa Miguu Tanzania (FAT) sasa TFF kwa vipindi viwili
tofauti. Pia aliwahi kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha
Waamuzi wa Mpira wa Miguu Tanzania (FRAT).
Vilevile
aliwahi kuwa mkufunzi wa waamuzi, mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF na
Mwenyekiti wa Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu Tanzania (FRAT) Mkoa
wa Pwani.
Kwa
upande wa vyama vya mpira wa miguu aliwahi kuwa kiongozi katika mikoa
ya Tabora, Pwani na wilayani Mpanda katika Mkoa wa Rukwa.
Msiba
wa Mkeremi uko nyumbani kwake Urambo, na kwa mujibu wa mtoto wake
Masoud Mkeremi, atazikwa Jumamosi kwenye makaburi ya Msafa yaliyoko
wilayani Urambo.
TFF
inatoa pole kwa familia na kuitaka kuwa na uvumilivu katika kipindi
hiki kigumu. Pia TFF itatoa ubani wa sh. 200,000 kwa familia ya marehemu
kama rambirambi zake.
Marehemu aliyekuwa akisumbuliwa na
presha na ugonjwa wa kisukari ameacha wajane wawili na watoto 12. Mungu
aiweke roho yake mahali pema peponi. Amina
HakiElimu waishauri Serikali, CWT kuhusu mgomo wa Walimu
Na Joachim Mushi, Thehabari.com
TAASISI ya HakiElimu nchini imeishauri Serikali pamoja na Chama Cha
Walimu Tanzania (CWT) kufikia makubaliano haraka iwezekanavyo, ili
kumaliza mgomo uliopo kwani waathirika zaidi na mgomo huo si wao bali ni
ni wanafunzi.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi
Mtendaji wa HakiElimu, Bi. Elizabeth Missokia alipokuwa akizungumza na
waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na mgomo wa walimu
unaoendelea maeneo mbalimbali nchini.
Alisema kila mwanafunzi ana haki ya kujifunza na kuelimishwa, kitu
ambacho hawakipati kwa sasa kutokana na mgomo wa walimu wanaoshinikiza
Serikali iwaongeze mishahara pamoja na kuwaboreshea mazingira ya kazi
zao.
Mkurugenzi huyo alisema kauli ya Serikali kudai haina uwezo wa
kuboresha maslahi na mazingira ya kazi ya watumishi wake haileti unafuu
wa maisha kwa watumishi wa umma hivyo kushauri iangalie namna ya
kufanya kumaliza mgogoro huo.
“HakiElimu inasisitiza kwamba nchi itafanikiwa kuboresha elimu
endapo tu itawekeza kwa walimu kwa kuboresha mazingira ya kazi, maslahi
ya walimu, kuwashirikisha walimu katika maamuzi kuhusu masuala ya elimu
na kuwapa walimu mafunzo kazini. Elimu bora haiwezi kuletwa na walimu
walio hoi,” alisema Missokia.
Aidha amewataka walimu kuhakikisha wanadai haki zao huku
wakiendelea kuwajibika kwa kufundisha na kuendeleza elimu yetu, kwani
wanamgogoro na Serikali na wala si wanafunzi na jamii kwa ujumla.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda Katika Maonyesho Ya NaneNane
Waziri mkuu, Mizengo Pinda akikagua mkungu
wa ndizi katika maonyesho ya wakulima Nanenane Mjini Morogoro Agosti
Mosi 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama
mzinga wa asili wa nyuki wadogo wakati alipotembelea banda la Magereza
kwenye maonyesho ya Wakulima Nanenane Mjini Morogo Agosti Mosi, 2012.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
No comments:
Post a Comment