MWIMBAJI WA THE VOICE ANAENDELEA VIZURI, KURUDI HOSPITALI HII LEO
Obed akiwa na Pastor Paul Safari wa DPC alipomtembelea nyumbani kumjulia hali. |
Mwimbaji wa kundi la The Voice la nchini bwana Obed John Mark ambaye alipata ajali jumatano iliyopita maeneo ya Sinza jijini Dar es salaam, hali yake inaendelea vizuri ambapo asubuhi ya leo anatarajia kuelekea hospitali ya rufaa ya Muhimbili kwa ajili ya uchukuaji wa kipimo cha T scan.
Akizungumza na GK, Obed amesema anamshukuru Mungu anaendelea vizuri kwasasa ingawa bado anasikia maumivu kwenye shingo licha ya kutumia dawa alizopatiwa na daktari Julius Dinda. Aidha mwimbaji huyo amesema ametoa shukrani zake kwa watu mbalimbali ambao wamekuwa wakifika nyumbani kwao kumjulia hali kitendo ambacho amesema amefarijika sana kuona kuna watu wanamjali.
Mwimbaji huyo alipata ajali maeneo ya Sinza Kamanyola wakati akielekea Magomeni, ambapo alirushwa hadi mtaroni na kuumia sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo mikono na miguu na hali yake kuelezwa kuwa haikuwa nzuri.Aidha kwa upande wa kundi hilo wakitoa taarifa za maendeleo ya mwimbaji huyo siku chache zilizopita wamesema;-
Mungu ni mwema wapendwa...hakika Mungu husikia sala zetu na zenu
pia....Dokta Julius Dinda kamshauri Obed kwa hizi siku mbili atumie dawa
alizompatia, then kama kutakuwa na mabadiliko yoyote basi arudi
hospitali kwenda kufanyiwa hicho kipimo cha T-Scan..Hakika Mungu
nakwenda kufanya kitu kwa mwenzetu Obed kupitia dawa alizopewa na dokta
Dinda na maombi yenu pia kwa hizi siku mbili..Tuzidi kumuombea mwenzetu
arudi katika hali yake ya kawaida kama ilivyo kuwa hapo awali...
The Voice. |
JIUNGE NA AGUSTINO KIHOMBO, NDANI YA OVERCOMERS FM RADIO
Jiunge na Agustino Kihombo
a.k.a A 2 K nadai ya Redio ya washindi
Overcomers fm Redio 98.6 kila siku za wiki kuanzia saa 07:00 hadi saa 09:30
asubuhi katika kipindi cha tujadili jumatatu hadi Ijumaa lakini pia katika
kipind cha Michezo na Burudani saa MOJA JIONO hadi saa MBILI kamili usiku.
Pia siku ya jumamosi katika
kipindi cha MIZANI kili jumamosi kuanzia saa 02:00 mchana hadi saa 04:00 jioni
katika mahojiano na ufafanuzi wa mada za kijamii,kisiasa na kiuchumi pamoja na
Uchambuzi wa michezo.
|
No comments:
Post a Comment