Tuesday, July 24, 2012


Rais Kikwete Akutana Na Dkt. Asha Rose Migiro

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa Dkt.Asha Rose Migiro ikulu jijini Dar es Salaam leo 


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha na kufanya mazungumzo na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa Dkt.Asha Rose Migiro ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akumuaga aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa Dkt.Asha Rose Migiro ikulu jijini Dar es Salaam leo. Chanzo: Freddy Maro

Mabasi ya Dar Express, Simba Mtoto yamegongana uso kwa uso eneo la Wami

Basi la Dar Express lililokuwa linatoka Arusha na basi la Simba Mtoto lililokuwa linaenda Tanga yamegongana uso kwa uso maeneo ya Wami. Mwanahabari wa "Globu ya Jamii" aliyekuwa eneo la tukio muda mfupi baada ya ajali kutokea anasema hadi anaondoka mahali hapo hakuna maafa ya watu kupoteza uhai yaliyoropotiwa ila, watu kadhaa wamejeruhiwa na kuna mtu mmoja amebanwa katikati ya mabasi ambayo kisa cha kugongana kwake bado hakijafahamika.

Majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika hospitali ya Chalinze.
Picture
Abiria wa wakishushwa kupitia madirishani
Picture
Abiria wakijaribu kumwokoa mwenzao aliyenaswa
Picture
Abiria wakiendelea na juhudi za kuwatoa wenzao

Maiti Mv Skagit zafikia 89



Idadi ya maiti za ajali ya kuzama kwa Meli ya MV Skagit zimeongezeka na kufikia 89 baada ya miili mingine 11 kupatikana leo katika maeneo manne tofauti ya  visiwa vidogovidogo vilivypo mwambao wa Zanzibar.

Afisa Habari Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar Inspekta Mohammed Mhina, amesema kuwa miili iliyopatikana leo, sita ni wanaume akiwemo kijana mdogo na mingine mitatu ya wanawake.
Inspekta Mhina amesema, maiti zote zimezikwa katika makaburi ya pamoja ya Kama yaliyopo nje kidogo ya mji wa Zanzibar chini ya usimamizi wa Jeshi la la Wananchi wa Tanzanaia JWTZ, Jeshi la Polisi, MKMK, JKU na Varantia.

Amesema miili hiyo ilipatikana katika viisiwa vya Pungume, Fumba, Chumbe na eneo linalokupwa na kujaa maji la Funguyasini maeneo jirani na kisiwa mama cha Unguja.

Naye Mkuu wa Polisi Kikosi cha Wanamaji na Bandari Zanzibar SP Martin Lisu, amesema kuwa kunauwezekano mkubwa kuwa maiti hizo zinaibuka kutoka katika meli hiyo ya Skagit.

Kamanda Lisu, amesema kuwa kutokana na kuendelea kuibuka kwa maiti hizo, Maafisa wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wanaendelea na zoezi lao la kutafuta miili mingine na kupokea taarifa za kuonekana kwa mwili kutoka kwa watu wenye vyombo binafsi vya uvuvi na kuzifuatilia.

Hivi karibuni akizungumza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete, Daktari Mkuu Mwelekezi wa Jeshi la Polisi nchini Dk. Ahamed Makata, alisema kuwa maiti nyungi zitaweza kupatikana ifikapo siku ya nne tangu kuzama kwa meli hiyo.

Alisema tabia ya maiti ya binadamu aliyekufa maji na kuzama, haiwezi kukaa chini ya maji kwa muda mrefu kama haikufungwa na kitu kizito kabla ya kuzama.

"Kwa kawaida maiti ya mtu aliyekufa maji haiwezi kukaa ndani ya maji wakati wote na kwamba hata kama itaendelea kubaki majini lakini katika muda wa kuanzia siku tatu na nne mwili ama miili hiyo nilazima ianze kuibuka na kuelea juu ya maji". Alisema Dk. Makata.

No comments:

Post a Comment