Tuesday, October 2, 2012



MBUNGE WA VITI MAALUM MKOAN IRINGA AAHIDI KUSHIRIKIANA NA WAZAZI WA WANAFUNZI WATAKAOSHINDWA KUENDELEA NA MASOMO YA KIDATO CHA NNE MWAKANI


Wazazi na walezi mkoani Iringa wameshauriwa kuwa karibu na watoto wao wa shule pamoja na kujenga mahusiano mazuri na walimu ili kujua maendeleo ya watoto wao pindi wanapokuwa shuleni.

Hayo yamesemwa na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Mh.Litha Kabati ambaye ndiye aliyekuwa Mgeni rasmi katika mahafari hiyo, akizungumza na wananchi pamoja na wanafunzi katika mahafari ya tatu ya kuhitimu kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Ipogolo iliyopo kata ya kitwiru manispaa ya Iringa na kuwataka wazazi kuacha tabia ya kuwaachia walimu pekee kuwa ndiyo waangalizi wa watoto hao badala yake washirikiane ili kuhakikisha wana tengeneza mazira yatakayo wafanya wanafunzi wasome kwa bidii.

Aidha Mh.Litha amewataka wanafunzi kujituma katika masomo yao pasipo kuangalia hali ya maisha katika familia zao wanamotokea kitendo ambacho kinaweza kuharibu malengo yao kimasomo,kauli hiyo imekuja baada ya kusomewa idadi ya wanafunzi wanaofaulu na kshindwa katika shule hiyo ambapo tangu kuanzishwa kwake mwaka 2007 na kufikia mwaka 2008 shule hiyo ilikuwa na kidato cha pili ambapo katika mtihani wao kati ya wanafunzi 160 wanafunzi 15 walipata C,75 D,57 F,na 13 ni watoro,2009 walikuwa 13walipata C,21 D,18 F,mwaka 2010 jumla ya wanafunzi 130 walifanya mtihani ambapo 1 alipata C,84 D,35 F, na 10 ni watoro na mwaka 2011 wanafunzi 112 walifanya mtihani 13 walipata C,23 D,61 F,na watoro walikuwa 12 na kwa upande wa kidato cha nne kwa mwaka 2010 -1 alipata Div III,4 Div IV,78 Div O na kwa mwaka 2011 wanfunzi 4 Div III,25 Div IV, 27 Div O, hali ambayo inaonesha mabadiliko ya kitaalima kwa muda wa mihula miwili iliyopita.

Pia ameahidi kushirikiana na wazazi wa wanafunzi wanaohitimu kidato cha nne pale wanaposhindwa kuwapeleka watoto wao shule hususani watoto wa kike ili kuongeza jitihada za kumkomboa mwanamke katika hali ya kukandamizwa katika maisha lakini pia kutatua baadhi ya changamoto zinazo ikabili shule kwa kushirikiana na wahisani wanao panda maendelea.

Akielezea changamoto zinazoikabili shule makamu Mkuu wa shule hiyo ya Sekondari Ipogolo Bi.Hilda Gadisau amesema shule hiyo inakabiliwa na upungufu wa maabara ya kujifunzi kwa masomo ya sayansi,ubovu wa madarasa,upungufu wa walimu pamoja na ukosefu wa Uzio wa shule hali inayowafanya wanafunzi kutoroka  kwa urahisi na kujiingiza katika makundi yasiyofa kama unywaji wa pombe pamoja na uchezaji wa kamali pamoja na upungufu wa vitabu vya masomo mbalimbali ukosefu wa jengo utawala ikijumuisha na nyumba za walimu.

Hivyo wameiomba serikali kuwasaidia kutatua baadhi ya changamoto zinazoikabili shule hiyo ilikuboresha maendeleo ya taaluma Shuleni hapo.

Picha zote hapo chini zinahusiana na tukio la mahafari ya kidato cha nne shule ya sekondari Ipogoro Mgeni rasmi ni Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Iringa hapo chini

Mh.Mb.Viti maalum mkoa wa IringaLitha Kabati

                   


















Wanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari Ipogoro










HS

No comments:

Post a Comment