Wednesday, March 12, 2014


TAHEA YAJITOSA KUWASAIDIA WANANCHI MKOANI IRINGA KUJITAMBU                     
Ili kusaidia jamii kuondokana na adui umasiki shirika la kitaalamu na kisayansi katika nyanja za Kilimo,Elimu, Maendeleo ya jamii na Ustawi wa jamii{Tanzania Home Economics Association(TAHEA)}limesema liko tayari kumsaidia  mtu binafsi, familia na jamii ya Tanzania kwa  ujumla  kijamii na kiuchumi kwa kutoa elimu ya fani mbalimbali.
Hayo yamesemwa na mratibu wa shilrika hilo bw Peter Mapunda,wakati alipokuwa akizungumzia mipango ya TAHEA,inayotekelezwa kwa sasa ambao ni Mpango wa kuhudumia watoto waishio katika Mazingira hatarishi.
   Mradi wa kuhudumia watoto waishio katika Mazingira hatarishi ngazi ya jamii katika wilaya ya Iringa  umefadhiliwa  na  watu wa Marekani kupitia shirika la Africare pamoja na mpango wa Kujengea uwezo AZAKI  unaotekeleza Mpango wa Pamoja Tuwalee wa kusaidia watoto waishio katika Mazingira hatarishi   mikoa ya Iringa Njombe, Dodoma na Singida
Aidha bw Mapunda amesema Katika huduma ya elimu ya  chakula na lishe watoto 6418 kati yao  wakike wakiwa 3105,walifikiwa kupitia walezi wao huku watoto  405 wakiume 205,na wakike 200  walisaidiwa chakula na watoto wengine 520,waliopo chini ya miaka mitano walihakikiwa kuangalia hali ya lishe.
Hata hivyo mratibu huyo ameongeza kuwa kwa mwaka 2013 walihamasisha uundwaji wa vikundi vya kuweka na kukopa  na vile vya uzalishaji mali pampja na kutoa elimu ya chakula na lishe.

CCM, Chadema waikaba NEC Iringa



Vyama vya siasa vilivyo na wagombea wake  katika jimbo la kalenga vimeaswa kuteuwa mawakala wanaoelewa hatua zote muhimu za uchaguzi vituoni  kuanzia hatua ya kufungua kituo hadi kutangaza matokeo,na tume imeandaa vitabu vidogo vya maelekezo kwa ajiri ya mawakala.
 Rai hiyo imetolewa na mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi Jaji mstaafu Damiani Lubuva wakiti alipokuwa akihutubia katika mkutano wa tume na viongozi wa vyama vya siasa uliofanyika katika ukumbi wa siasa ni kilimo manispaa ya iringa,ambapo amesema kuwa ni vyema viongozi wa vyama vya siasa wakateu mawakala toka katika eneo husika ili kutambua vyema uhalali wa wapiga kura.
 Aidha amesisitiza kwa vyama vya siasa kuacha kutumia lugha zenye maneno ya uchochezi na uvunjivu wa amani,na wawaase wananchi kuondoka eneo la kupigia kura mara baada ya kupiga kura kwani kura zitakuwa salama kwakuwa kutakua na ulinzi wa kutosha hivyo  sio kila mmoja ataweza kufika katika eneo la kupigia kura bila utaratibu .
 Katika mkuno huo uliohudhuliwa na wadau mbalimbali akiwemo kamanda wajeshi la polisi mkoa wa iringa,kiongozi wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA,ndicho kilicho anza kuchangia ambapo mwakilishi wake Singo Kigaila ambae ni mkuu wa kampeni wa chama hicho amesema kumekuwa na tofauti katika daftari la wapiga kura kuwa imeoneka katika kituo cha kaningo’mbe wameongezeka wapiga kura watatu,ambapo hali hiyo imejitokeza pia katika vituo vingine kati ya vituo vyote 216,vya kupgia kura.
 Akijibu hoja hiyo naibu katibu wa tume na mkuu wa IT,Dr Sisti Karia,amesema hali hiyo ilijitokeza kutoka na marekebisho  ya kasoro ikiwamo kwa wale waliojiandikisha zaidi ya mara moja pamoja na wale waliojiandikisha mwaka 2010,na hawakuwekwa kwenye kumbukumbu hizo ndio imepelekea mabadiliko hayo.
 Kwa upande wa mwakilishi wa chama cha mapinduzi CCM,katibu wa ccm wilaya ya mufindi bw Miraji Mtatulu ambae pia mratibu wa kampeni za chama hicho,amesema ni vyema uongozi wa tume ukakaa tena na viongozi wa vyama siasa ili wakaangile tatizo hilo la kuongozeka au kupungua kwa idadi ya wapiga kura na wakatoa tamko la pomoja .
 Akizungumzia hali ya usalama katika shughuli nzima ya kampeni,kupiga kura hadi kutangazwa kwa matokeo kamanda wa polisi mkoani iringa Ramadhani Mungi amesema siku ya kupiga kura hatawavumilia ama kuwa ruhusu vikundi vya ulinzi vya Grini gadi au redi gadi kuwepo eneo la kupgia kura,na atahakikisha hakuna gari yoyote itakayo husika kubeba wapiga kura kwa namna ya kushawishiwa na mtu au chama chochote.

Vyama vya siasa vilivyo na wagombea wake  katika jimbo la kalenga vimeaswa kuteuwa mawakala wanaoelewa hatua zote muhimu za uchaguzi vituoni  kuanzia hatua ya kufungua kituo hadi kutangaza matokeo,na tume imeandaa vitabu vidogo vya maelekezo kwa ajiri ya mawakala.
 Rai hiyo imetolewa na mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi Jaji mstaafu Damiani Lubuva wakiti alipokuwa akihutubia katika mkutano wa tume na viongozi wa vyama vya siasa uliofanyika katika ukumbi wa siasa ni kilimo manispaa ya iringa,ambapo amesema kuwa ni vyema viongozi wa vyama vya siasa wakateu mawakala toka katika eneo husika ili kutambua vyema uhalali wa wapiga kura.
 Aidha amesisitiza kwa vyama vya siasa kuacha kutumia lugha zenye maneno ya uchochezi na uvunjivu wa amani,na wawaase wananchi kuondoka eneo la kupigia kura mara baada ya kupiga kura kwani kura zitakuwa salama kwakuwa kutakua na ulinzi wa kutosha hivyo  sio kila mmoja ataweza kufika katika eneo la kupigia kura bila utaratibu .
 Katika mkuno huo uliohudhuliwa na wadau mbalimbali akiwemo kamanda wajeshi la polisi mkoa wa iringa,kiongozi wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA,ndicho kilicho anza kuchangia ambapo mwakilishi wake Singo Kigaila ambae ni mkuu wa kampeni wa chama hicho amesema kumekuwa na tofauti katika daftari la wapiga kura kuwa imeoneka katika kituo cha kaningo’mbe wameongezeka wapiga kura watatu,ambapo hali hiyo imejitokeza pia katika vituo vingine kati ya vituo vyote 216,vya kupgia kura.
 Akijibu hoja hiyo naibu katibu wa tume na mkuu wa IT,Dr Sisti Karia,amesema hali hiyo ilijitokeza kutoka na marekebisho  ya kasoro ikiwamo kwa wale waliojiandikisha zaidi ya mara moja pamoja na wale waliojiandikisha mwaka 2010,na hawakuwekwa kwenye kumbukumbu hizo ndio imepelekea mabadiliko hayo.
 Kwa upande wa mwakilishi wa chama cha mapinduzi CCM,katibu wa ccm wilaya ya mufindi bw Miraji Mtatulu ambae pia mratibu wa kampeni za chama hicho,amesema ni vyema uongozi wa tume ukakaa tena na viongozi wa vyama siasa ili wakaangile tatizo hilo la kuongozeka au kupungua kwa idadi ya wapiga kura na wakatoa tamko la pomoja .
 Akizungumzia hali ya usalama katika shughuli nzima ya kampeni,kupiga kura hadi kutangazwa kwa matokeo kamanda wa polisi mkoani iringa Ramadhani Mungi amesema siku ya kupiga kura hatawavumilia ama kuwa ruhusu vikundi vya ulinzi vya Grini gadi au redi gadi kuwepo eneo la kupgia kura,na atahakikisha hakuna gari yoyote itakayo husika kubeba wapiga kura kwa namna ya kushawishiwa na mtu au chama chochote.

No comments:

Post a Comment