Tuesday, June 3, 2014

Wajasiliamali wanufaika na uwepo wa MUCOBA Bank Iringa



 BENKI YA WANANCHI MUFINDI (MuCoBa)NI KIVUTIO KWA WAJASLIAMALI NYANDA ZA JUU KUSINI
 
Meneja Mkuu Mpya wa Benki ya MUCOBA Bw Ben Mahenge akisoma taarifa ya benki kwa wanachama wa benki hiyo

Mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa MUCOBA BENKI Bi Marcellina Mkini baada ya kuwasilisha taarifa ya meneja wa wanahisa
Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Everlista Kalalu akizungumza na wanachama wa hiza za MuCoBa Benki
Wanachama na wanahisa wa MuCoBa

Benki ya wananchi Mufindi(MuKoBa) imeendelea kuimarisha huduma zake ili kiwarahisishia wananchi wa mkoa wa Iringa kutunza fedha na mikopo rafiki.
Haya yamesemwa katika taarifa ya iliyowasilishwa kwa wanachama wa Benki hiyo katika mkutano mkuu uliofanyika mjini Mafinga  ikiwasilishwa kwa niaba ya mwenyekiti wa bodi ya Benki hiyo Bw Attilio Mohele mjumbe wa Bodi hiyo Bi Marcellina Mkini amesema wananchi wameendelea kunufaika na huduma za MuKoba huku akielezea mafanikio yanayopatikana kutokana na uboreshaji wa huduma.
Amesema wameendelea kutoa huduma za akiba na mikopo kwa kuongeza mwitikio wa uwekaji wa akiba na utumaji wa fedha,bima na matumizi ya teknolojia inayorahisisha huduma hiyo kwa wananchi wa mkoa wa Iringa kwa wakati pia ameelezea mikakati ya kushirikiana na wadau mbalimbali katika utoaji wa huduma za kifedha ili kurahisha huduma kwa jamii.
Aidha Bi Mkini ameelezea changamoto zinazokwamisha maendeleo ya huduma hiyo kuwa ni pamoja na ugumu wa upatikanaji wa vibali vya mbao na kushuka kwa bei za mbao kutokana na ushindani,udogo wa mtaji,mkopo chechefu na gharama kubwa ya kufikisha huduma ya fedha kwa wananchi walipo vijijini.
Hivyo amewataka wananchi kuwa wavumilivu pindi wanapokuta na changamoto pindi wanapoenda kupata huduma za kifadha katika benki hiyo kwani lengo la MuKoBa ni kuwasadia wananchi wa mkoa wa Iringa.
 



SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI IMEKUWA TISHIO KWA WANAWAKE NCHINI
Mkurugenzi wa T-Marc Tanzania Diana Kisaka akizindua mradi wa kupambana na saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawake mkoani Iringa.
 Katibu Tawala wa mkoa wa Iringa na aliyekuwa mgeni rasmi  wakati wa uzinduzi huo Wamoja Ayubu akitoa maoni yake
 Wanawake   Mkoani  Iringa  wametakiwa  ,  kuchukua tahadhari hatua kwa  kupima  magonjwa mbalimbali ikiwemo saratani  ya mlango  wa kizazi, ugonjwa  unaoonekana kuwa tishio kwa wanawake  Wengi  hapa nchini.

Akizungumza  na Mtandao huu ofisini kwake  Mwenyekiti  wa mabalozi wa wahudumu wa kujitolea  katika  shirika la  (TALWORK) Mkoani Iringa  Bw Nasri  Mwampeta  amesema kuwa takwimu zinaonyesha  kuwa wanawake 2  hufariki kila mwezi Mkoani Iringa  kutokana na ugonjwa huo ambapo kwa mwaka hufariki  24.

Amesema kuwa  ugonjwa  huo unatokana na  virusi  aina ya  Human  Papiloma Virus (H.P.V) ambavyo huambukizwa  kwa njia ya kujamiiana.

Aidha  amesema kuwa   ugonjwa huo  unawapata wanawake  walio na umri  wa miaka (25-50) ambapo hauna dalili  kwani hukaa  miaka  (10-20)  baada ya hapo ndipo dalili zinaanza kujitokeza.

Ametaja visababishi  vya  ugonjwa huo kuwa ni utumiaji wa  bidhaa za tumbaku, kuzaa watoto zaidi  ya watano, kujamiiana katika umri mdogo ambapo amesema kuwa  wanaoishi na virusi vya ukimwi  wana uwezekano  mkubwa wa kupata saratani.

Amewataka wanawake  kujitokeza kwa  wingi  kupima  kwani ugonjwa huo unatibika  bila  gharama yoyote  katika vituo mbalimbali Mkoani Iringa  ikiwemo Hospitali ya Mkoa,   kituo  cha  afya Ipogoro,  Marie   Stopers  na hospitali ya Ipamba.

No comments:

Post a Comment