Wednesday, June 4, 2014

UONGOZI MPYA WA TFF CHINI YA RAIS MALINZI WAMUINUA MVERA KUWA MKURUGENZI WA WANACHAMA WA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI

ALIYEKUWA KATIBU WA CHAMA CHA SOKA MKOA WA IRINGA ELIUDI MVELLA WAMAHANJI AJIUZULU RASMI ,SASA NI MATAWI YA JUU....
Malinzi ninaimani na Mvella atatumia uzoefu wake wa muda mrefu katika uongozi wa mpira wa miguu kuhakikisha TFF inaimarisha uhusiano wake na wanachama wake.
TFF ina wanachama 44 ambao ni vyama vya mpira wa miguu vya mikoa, vyama shiriki na klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL).

Aliyekuwa katibu wa chama cha mpira wa miguu mkoa wa Iringa Eliud Mvella Wamahanji ambae amejiuzulu nafasi hiyo rasmi 
Wamahanji  katikati akizungunza na wanahabari mkoa wa Iringa  sababu za kujiuzulu kwake 
Wanahabari mkoa  wa Iringa wakimsikiliza aliyekuwa katibu wa chama  cha soka mkoa wa Iringa Eliud Mvela Wamahanji kulia alipotangaza kujiuzulu nafasi yake 
Wamahanji  akiwashukuru  wanahabari Iringa kwa ushirikiano wao mkubwa 

Wamahanji  akimtambulisha katibu wake msaidizi Bw Ambwene ambae atakaimu nafasi yake hadi uchaguzi mdogo utakapofanyika 

>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

ALIYEKUWA katibu  wa chama cha soka mkoa wa Iringa Eliud Mvella Wamahanji ametangaza rasmi  kujiuzulu nafasi hiyo na kuahidi makubwa katika  kuinua soka hapa nchini.

Sababu kubwa ya  kuitana  hapa ni kutaka  kuwaaga baada ya  kuamua kujiuzulu nafasi ya ukatibu mkoa  wa Iringa baada ya TFF kuniteua kuwa mkurugenzi msaidizi wa sheria na uanachama wa TFF nitakayosimamia kitengo cha  wanachama 44 wa TFF .
Wamahanji  alisema  kuwa baada ya  TFF kumuona anafaa kuongoza nafasi hiyo binafsi ameamua  kujiuzulu nafasi hiyo japo haikuwa lazima  kuachia ngazi nafasi hiyo.

Alisema  kuwa ni mengi amepata  kuyafanya katika soka la Tanzania na mkoa  wa Iringa na  hivyo anatambua  kuondoka kwake ni sehemu ya mafanikio ya  jitihada zake katika  kuendeleza soka la Tanzania na  kuwa hata atakapokwenda TFF katika nafasi hiyo aliyopewa atahakikisha anaendelea  kufanya  vema zaidi.

"kubwa ambalo  nimefanikiwa katika uongozi wangu ni kuzalisha  waamuzi 15  katika mkoa  wa Iringa pamoja na kuziwezesha  timu  mbili za mkoa  wa Iringa Kurugenzi na Lipuli Fc kucheza  ligi daraja kwanza"

Hata  hivyo alisema  kuwa mbali ya mafanikio hayo  pia suala la mahusiano kati ya vyombo  vya habari na serikali ya mkoa kuna  vimeendelea  kuwa pamoja .

Aidha  alisema jitihada nyingine  alizozifanya ni kuanza makakati wa ujenzi wa uwanja wa kisasa wa nyasi za bandia katika Manispaa ya  Iringa uwanja  utakaojengwa eneo la Kitwiru chini ya ufadhili wa FIFA na TFF na kuwa jitihada za ujenzi zinaendelea kufanyika na Manispaa ya Iringa tayari  imetoa eneo .

No comments:

Post a Comment