Wednesday, June 4, 2014



 WALEMAVU WAASWA KUJISHUGHULISHA BAADALA YA KUWA TEGEMEZI
Katibu wa chama cha walemavu wa macho  Wasioona    katika manspaa ya iringa David mgimwa  amewataka walemavu wenzake    kutotegemea misaada kutoka kwa serikali bali wajishughulishe kwa kile kidogo wanacho kipata.

Akizungumza  katika kikao chao kilichofanyika katika ofisi za walemavu wa macho mjini iringa bwana David Mgimwa ameeleza kuwa anaomba ushirikiano na serikali kwaajili ya kuanzisha chanzo cha mapato endelevu kitakacho kuwa kinasaidia walemavu kimaisha.

Wakati huohuo Bw mgimwa ameomba misaada kutoka kwa mashirika mbalimbali pamoja na serikali ili kujenga kituo kikubwa cha kulelea walemavu hao pamoja na kituo cha kutolea huduma ya elimu.

Aidha Katibu  huyo    ameongeza   kwa kusema kuwa anawashauri walemavu wote wenye uwezo kidogo kuacha kutegemea misaada kila wakati  bali wajishughulishe na sekta mbalimbali za kiuchumi kwa kile wanacho kipata kutoka serikalini na taasisi binafsi.

No comments:

Post a Comment