Thursday, June 5, 2014

MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA YAFANA IRINGA TAZAMA

WANANCHI IRINGA WAPONGEZWA KWA UTUNZAJI WA MAZINGIRA
Mkuu wa wilaya ya Kilolo Gerad Guninita pamoja naye katibu tawala mkoani Iringa Wamoja Ayubu wakiwa katika mkutano wa mazingira
Baadhi ya vitu vya maonesho katika siku ya maadimisho ya mazingira yaliyofanyika Iringa mjini viwanja vya Mwembetogwa
Wanafunzi nao hawakuwa nyuma kuadhimisha siku hiyo
Wakati  dunia nzima  leo  ikiazimisha siku ya mazingira  wananchi  Mkoani Iringa wametakiwa kuendeleaa kuyatunza,na  kuyaweka katika hali ya usafi na ya kuridhisha  ambapo kwa mwaka huu Mkoa wa Iringa umeshika nafasi ya kwanza kwa usafi  kitaifa.
Akizungumza  na wananchi  kwa niaba ya mkuu wa Mkoa katika  viwanja vya Mwembetogwa  Mkuu wa wilaya ya kilolo Bw Gerald  kuninita  amesema kuwa yeyote  atakayeharibu  mazingira ikiwemo ulimaji holela katika  vyanzo vya maji achukuliwe hatua  huku  akiwataka wananchi  kuacha uwindaji  haramu, kutunza  misitu ya asili, kuhakikisha kila  kaya inapanda  miti isiyopungua 10 kila mwaka na kuwafichua  wale wote wanaoanzisha moto kichaa katika mazingira.
Aidha  amesema kuwa  kila  wilaya   iandae taarifa ya  uzuiaji moto kichaa hasa  kipindi cha kiangazi  kwani  uchomaji misitu unarudisha nyuma uhifadhi wa mazingira  ambapo atakayebainika kufanya  hivyo kulingana na kifungu  cha  sheria ya misitu no 12  atatozwa faini ya sh laki 3  na kanuni ya sheria ya makosa ya jinai kifungu no 21 na 22  kitatoa adhabu ya kifungo cha miaka isiyopungua 14  kwa atakayekiuka  taratibu hizo.
Naye  Meya wa Manispaa ya Iringa  Bw Amani Mwamwindi amekiri Mkoa wa Iringa kushika nafasi ya kwanza kitaifa katika usafi  na kueleza vitu vilivyopelekea kushika nafasi hiyo kuwa ni upandaji wa miti, maua, mpangilio mzuri wa nyumba za watu, vyuo, shule pamoja na zahanati.
Ikiwa ni mara ya kwanza  Mkoa  wa Iringa  kushika  nafasi hii ambayo miaka kadhaa imekua ikishikiliwa na wilaya ya Moshi iliyopo Mkoani Kilimanjaro wakazi mbalimbali Mkoani Iringa  wameonyesha  kuguswa na  suala hili  pamoja na kupongeza juhudi  zilizofanywa  mpaka kufikia hatua hii na kuahidi kuyatunza mazingira na kuhakikisha yanakuwa katika hali ya usafi.



No comments:

Post a Comment