Wednesday, June 27, 2012



ELIMU YETU YA TANZANIA INAKWENDA WAPI?


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi  Dk.Shukuru Kawambwa

Hivi ni kweli kuwa elimu ni ngumu ama mfumo wa elimu tuliojiwekea hapa kwetu ndo unaoleta ugumu katika swala zima la elimu TANZANIA?

Mimi sijui, lakini yale ninayo yasikia kutoka kwa watu mbalimbali ndo yaliyonifanya mimi hadi kufikia kujiuliza swali kama hili.vijana wengi waliopo mashuleni na vyuoni wamekuwa wakilalamika juu ya ugumu wanaokutana nao katika masomo yaho hadi kufikia kusema kuwa elimu ni ngumu.huku ugumu huu ukionekana kuongezeka na kiwango cha ufaulu kupungua sambamba na mabadiliko mbalimbali katika mitaala ya kufundishia wapo waliojaribu kusema itakuja kufika siku TANZANIA kuongozwa na mtu mwenye ufaulu wa kiwango cha zero kabisa.huku shule za serikali zikionekana kuboronga kwa wingi hasa hizi za kata wanafunzi wanaotoka katika shule hizo

wamedai kuwa ukosefu wa vifaa vya kufundishia pamoja na walimu kutoingia kwenye vipindi ndiko kunakochangia wao kufanya vibaya.

kwa uchunguzi mdogo tu walimu wengi wamekuwa wakiacha kufundisha na wanapo ulizwa kwanini wanafanya hivyo hudai ni kutokana na kutolipwa mishahara yao kwa wakati jambo linalowafanya wao kuwa na maisha magumu huku wengi wao wakiwa ni wapangaji katika nyumba za watu binafsi..kitu kinacho wafanya wengi wao kufungua masomo ya ziada ama kwa jina lingine tution ili waweze kupata fedha za kujikimu na mahitaji yao na hapo ndipo wale wanafunzi waliopo shule hujikuta hawasomi kwani mwalimu hayupo shule bali kwenye kituo chake cha kufundishia masomo ya ziada na ndipo wale wenzangu na mimi wasio na uwezo wa kulipia masomo hayo hujikuta wameachwa njiani..sasa kwa mfano mdogo kama huu ni kweli kuwa elimu ni ngumu ama mfumo wa elimu ndo mgumu? Hii ni changamoto tosha kwa selikari yetu kuhakikisha inaliweka sawa hili ili kuleta tija kwa wanafunzi na kufanya kiwango cha ufaulu kuongezeka.

Baadhi ya watu wamekuwa wakichangia kupitia kipindi cha tujadili kinachorushwa na Overcomers Fm Redio kuanzia saa moja kamili hadi saa tatu asubuhi kuhusiana na chamoto ambazo walimu katika sektam ya elimu wamekua wakikabiliwa nayo ni pale tu wanapo kosa kuthaminiwa lakini pia serikali kushindwa kuwapa kipao mbele katika mishahara na kuwafanya walim kuanza kujishughulisha na mambo yatakayo waletea mafanikio kuliko kusubiri ahadi za serikali zisizo tekelezeka kwa wakati,Nini cha kufanya ni serikali kuwa thamini walim na kutambua kama ilivyo kwa sekta zingine kama vile afya,kilimo,maji umeme na nyinginezo

No comments:

Post a Comment