Thursday, December 12, 2013


 WALIMU IRINGA NA KILOLO WASHAURIWA KUJIUNGA NA ASASI ZA FEDHA ILI KUJIKWAMUA NA WIMBI LA UMASKINI
Zaidi ya shilingi milioni  mia saba tisini na sita,imetolewa kwa wanacha wapatao 494 wa   chama cha walimu cha akiba na mikopo{IRINGA  RURAL TEACHERS SACCOS},kama mkopo kutoka katika chama hicho ili kuwanufaisha wanachama wake.
         
Hayo yamebainishwa na mwenyekiti wa chama hicho bw Abass Kamote,wakati alipokuwa akiwasilisha taarifa ya chama katika mkutano mkuu wa 16 wa chama hicho,ambapo pia walijadili taarifa mbalimbali ya kamati ya usimamizi ya mwaka 2013,uliofanyika katika ukumbi was t dominic manispaa ya iringa desemba 11 mwaka huu.

Aidha mwenyekiti huyo ameongeza kuwa licha ya uwepo wa changamoto mbalimbali katika chama hicho,wamefanikiwa kuboresha hali zao za kijamii na kiuchumi,ikwamo ujenzi wa nyumba bora za wanachama 152,kutoa mikopo ya sh 796,650,000 kwa wanachama 494,pamoja na kuwa saccos bora kwa saccos za mikoa ya irinmga na njombe.

Kwa upande wake bw Martin Simango,akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi,waziri wa fedha mh William Mgimwa,ambae pia ni mbunge wa jimbo la kalenga,amesema kuwa ni vyema mwanachama awe mwaminifu katika kufanya marejesho,na kila mwalimu ajiunge na chama hicho.

Hata hivyo ameongeza kuwa mh waziri yupo tayari kuweza kukikopesha chama hicho,ili kila mwanachama aweze kupata mkopo kwa wakati,na kuondoa adha ya kusubiriana katika kuchukua mikopo.

No comments:

Post a Comment