Tuesday, June 10, 2014

Maadhimisho ya uchangiaji wa damu salama kufanyika Viwanja vya mwembetogwa manispaa ya Iringa..



MKUU WA MKOA WA IRINGA: 
WANANCHI JITOKEZENI KUCHANGIA DAMU
 
Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma akizungumza na wanahabari juu ya maadhimisho ya Uchangiaji wa damu salama.
Wananchi  Mkoani Iringa  wameombwa  kujitokeza katika maadhimisho ya siku ya kuchangia  damu kwa hiyari  ili kunusuru  maisha  ya  wagonjwa  wanaopungukiwa na damu mkoani hapa.

Wito huo umetolewa na Mkuu  wa  mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma wakati akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake amesema kuwa  kampeni  hiyo ya uchangiaji damu ilianza june 1 na itamalizika tar 14 June  mwaka huu katika  viwanja  vya Mwembe  Togwa  ikiwa lengo kubwa  ni kuwa na hazina  kubwa ya damu ya kutosha  katika  hospitali ya Rufaa.
Amesema pamoja na maadhimisho hayo ambapo mkoa wa Iringa umebahatika kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo ya siku ya uchangiaji wa damu duniani kikanda ikiwa imebeba kauli mbiu inayosema “DAMU SALAMA UHAI WA MAMA”(SAFE BLOOD FOR SAVING MOYHERS)

Aidha ametanabaisha kuwa vifo vingine vya akina mama katika Hospitali nyingi hapa nchini husababishwa na ukosefu wa damu iliyo salama hivyo kila mtu aguswe na hilo kwani hakuna kama mama.
Pia Dr Ishengoma ameyataja makundi yanayohitaji damu kuwa na pamoja na watoto wadogo waliochini ya umri wa miaka mitano (50%),wajawazito na wanawake wenye matatizo ya uzazi (30%),Majeruhi wa ajali mbalimbali hasa ajali za barabarani na watu wanaofanyiwa tiba ya upasuaji(15%) na wale wote wenye magonjwa mbalimbali yanayosababisha upungufu wa damu(5%)

Hivyo amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi katika siku hizo za maadhimisho ili kuonesha ushirikiano na kuchangia damu ambayo na uhai wa mama.

Kwa upande wake meneja wa Damu salama salama kanda ya nyanda za juu kusini Dr Kokuhabwa Nukuras Amesema  kuwa  jopo la wataalam wa damu tayari limewasli mkoani Iringa ili kufanikisha maadhimisho hayo ikiwa ni pamoja na kupita katika baadhi ya maeneo kuzungumza na jamii ikiwemo mashuleni na vyuoni huku wakihamasisha kujitokeza katika uchangiaji huo wa damu.
 
Dr Kokuhabwa Nukuras Menejawa Damu salama Kanda ya nyanda za juu kusini
Aidha Dr Kokuhabwa amesema kwa kuwa katika ukanda wa kusini  hazina ya damu iko Mkoani Mbeya  hivyo imekuwa  ikileta usumbufu  pindi  wanapopungukiwa  na damu  katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa hivyo jambo linalofanyika ni kukusanya damu ili kuwepo na hazina ndogo ya damu mkoani hapa.
Pia Dr Kokunabwa amesema changamoto iliyopo ni elimu duni kwa jamii juu ya uchangiaji wa damu salama.

Hivyo amewaomba wananchi kuwa wazalendo  katika tukio hilo  kwani  watapimwa kwanza  ndipo zoezi litaendelea  ambapo amewataka  wananchi kujitokeza kwa wingi  ili hazina ya Mkoa wa Iringa iwe na damu ya kutosha.

No comments:

Post a Comment