VIJANA WA VIKAE IRINGA WAPEWA SEMINA YA UJASILIAMALI
KIJANA.COM
ELIMU BORA KWA VIJANA SHIRIKI KUIFIKISHA
Friday, June 20, 2014
Tuesday, June 17, 2014
MTOTO WA AJABU AZALIWA MAKETE
Mtoto wa ajabu amezaliwa huko wilayani makete mkoani njombe usiku wa kuamkia tarehe kumi na saba june 2014.
Ukimuona
mtoto ngozi yake ni kama amevaa koti kubwa kushinda uwezo wa mwili wake
akiongea na blog hii reporter Daima kyando alisema mtoto huyo wa ajabu
alikua na tumbo kubwa lililomeza viungo vingine vya mwili kama
miguu,mikono,kiuno na shingo.
Habari
zaidi zinasema kuwa mtoto huyo alizaliwa akiwa amekwisha fariki na
alizaliwa kwa njia ya upasuaji,chanzo cha tatizo la mtoto huyo
hakikuweza kufahamika mara moja mpaka tunaenda mtandaoni madaktari
walikuw wakiendelea na uchunguzi.
Mama wa mtoto huo hakuweza kuongea lolote zaidi alilia kwa uchungu kwani na yeye alishikwa na bumbuazi juu ya kilichotokea akihisi ni ndoto.
ukimuangalia zaidi mtoto huyo unaweza kugundua kuwa ana umbo la chura,eeeeh mungu heal the world.
Tuesday, June 10, 2014
Maadhimisho ya uchangiaji wa damu salama kufanyika Viwanja vya mwembetogwa manispaa ya Iringa..
MKUU WA MKOA WA IRINGA:
WANANCHI JITOKEZENI KUCHANGIA DAMU
![]() |
Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma akizungumza na wanahabari juu ya maadhimisho ya Uchangiaji wa damu salama. |
Wananchi
Mkoani Iringa wameombwa kujitokeza katika maadhimisho ya siku ya kuchangia
damu kwa hiyari ili kunusuru maisha
ya wagonjwa wanaopungukiwa na damu mkoani hapa.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Christine Ishengoma wakati akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake amesema kuwa kampeni hiyo ya uchangiaji damu ilianza june 1 na itamalizika tar 14 June mwaka huu katika viwanja vya Mwembe Togwa ikiwa lengo kubwa ni kuwa na hazina kubwa ya damu ya kutosha katika hospitali ya Rufaa.
Amesema pamoja na maadhimisho hayo ambapo mkoa wa
Iringa umebahatika kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo ya siku ya uchangiaji wa
damu duniani kikanda ikiwa imebeba kauli mbiu inayosema “DAMU SALAMA UHAI WA MAMA”(SAFE BLOOD FOR SAVING MOYHERS)
Aidha ametanabaisha kuwa vifo vingine vya akina
mama katika Hospitali nyingi hapa nchini husababishwa na ukosefu wa damu iliyo
salama hivyo kila mtu aguswe na hilo kwani hakuna kama mama.
Pia Dr Ishengoma ameyataja makundi yanayohitaji
damu kuwa na pamoja na watoto wadogo waliochini ya umri wa miaka mitano
(50%),wajawazito na wanawake wenye matatizo ya uzazi (30%),Majeruhi wa ajali
mbalimbali hasa ajali za barabarani na watu wanaofanyiwa tiba ya upasuaji(15%)
na wale wote wenye magonjwa mbalimbali yanayosababisha upungufu wa damu(5%)
Hivyo amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi
katika siku hizo za maadhimisho ili kuonesha ushirikiano na kuchangia damu
ambayo na uhai wa mama.
Kwa upande wake meneja wa Damu salama salama kanda
ya nyanda za juu kusini Dr Kokuhabwa Nukuras Amesema kuwa jopo
la wataalam wa damu tayari limewasli mkoani Iringa ili kufanikisha maadhimisho
hayo ikiwa ni pamoja na kupita katika baadhi ya maeneo kuzungumza na jamii
ikiwemo mashuleni na vyuoni huku wakihamasisha kujitokeza katika uchangiaji huo
wa damu.
Aidha Dr Kokuhabwa amesema kwa kuwa katika ukanda
wa kusini hazina ya damu iko Mkoani Mbeya hivyo imekuwa
ikileta usumbufu pindi wanapopungukiwa na damu
katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa hivyo jambo linalofanyika ni
kukusanya damu ili kuwepo na hazina ndogo ya damu mkoani hapa.
Pia Dr Kokunabwa amesema changamoto iliyopo ni
elimu duni kwa jamii juu ya uchangiaji wa damu salama.
Hivyo amewaomba wananchi kuwa wazalendo katika tukio hilo kwani
watapimwa kwanza ndipo zoezi
litaendelea ambapo amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi ili hazina ya Mkoa wa Iringa iwe na damu ya
kutosha.
Friday, June 6, 2014
MRADI WA SHICS KUZINDULIWA KUTUNZA UTAMADUNI WA NYANDA ZA JUU KUSINI
MRADI WA SHICS KUZINDULIWA KUTUNZA UTAMADUNI WA NYANDA ZA JUU KUSINI
Chifu wa kabila la wahehe Abdul Adam Sapi(Mfwimi) akizunguza katika mkutano wa uzinduzi wa mradi wa SHICS katika viwanja vya mwembetogwa |
Meneja wa mradi wa SHICS wa tatu kulia aliyejifunga nguo nyeupe |
Mhifadhi Mkuu wa hifadhi ya Ruaha Christoph Timbuka(Katikati) |
Mradi wa Utamaduni uitwao 'Fahari Yetu' wazinduliwa Nyanda za juu kusini leo katika viwanja vya Mwembetogwa Mkoani Iringa.
Akizinduzi
Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo Mhifadhi Mkuu wa hifadhi ya Ruaha
Christoph Timbuka kwa Niaba ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Nchini Tanzania amekipongeza Chuo Kikuu cha Iringa Kupata Mradi huo na
kuwashukuru Umoja wa Ulaya kwa kuwafadhili kwa miaka hiyo Mitano.
Timbuka ameuomba mradi huo kuendelea pindi ufadhili
huo utakapoisha ili watanzania wapate kunufaika zaidi kupitia mradi huo katika kudumisha utamaduni Nchini Tanzania.(MM)
Naye Meya wa Manispaa ya Iringa Amani Mwamwindi ameutaka mradi huo
kuenzi mila na desturi ili kutuza Historia ya Nchi ya Tanzania.
Kwa upande wake Meneja wa Mradi wa Fahari Yetu Jan Kuever amesema kuwa, lengo la mradi
huo ni kusaidia vijana kupata ajira, kupunguza umasikini kwa kuongeza
mapato katika nyanja ya utalii kwa kuelimisha wananchi wa nyanda za juu
kusini kutembelea vyanzo mbalimbali vya utamaduni uliomo Nchini
Tanzania.
Ameongeza
kuwa, Mradi huo umeshirikisha watu mbalimbali kikiwemo Chuo Kikuu cha
Iringa, TANAPA, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Manispaa ya Iringa pamoja na
wananachi kwa ujumla.
Aidha,
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa Prof. Nicholas Bangu ameshukuru kupata
mradi huo kupitia Shirika la Umoja wa Ulaya na kuahidi kuendeleza mradi
huo pindi mkataba utakapoisha kwani ni ufadhili wa miaka mitano kuanzia
sasa.
Thursday, June 5, 2014
MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA YAFANA IRINGA TAZAMA
WANANCHI IRINGA WAPONGEZWA KWA UTUNZAJI WA MAZINGIRA
![]() |
Mkuu wa wilaya ya Kilolo Gerad Guninita pamoja naye katibu tawala mkoani Iringa Wamoja Ayubu wakiwa katika mkutano wa mazingira |
![]() |
Baadhi ya vitu vya maonesho katika siku ya maadimisho ya mazingira yaliyofanyika Iringa mjini viwanja vya Mwembetogwa |
![]() |
Wanafunzi nao hawakuwa nyuma kuadhimisha siku hiyo |
Wakati dunia
nzima leo ikiazimisha siku ya mazingira wananchi
Mkoani Iringa wametakiwa kuendeleaa kuyatunza,na kuyaweka katika hali ya usafi na ya
kuridhisha ambapo kwa mwaka huu Mkoa wa
Iringa umeshika nafasi ya kwanza kwa usafi
kitaifa.
Akizungumza
na wananchi kwa niaba ya mkuu wa
Mkoa katika viwanja vya Mwembetogwa Mkuu wa wilaya ya kilolo Bw Gerald kuninita
amesema kuwa yeyote
atakayeharibu mazingira ikiwemo
ulimaji holela katika vyanzo vya maji
achukuliwe hatua huku akiwataka wananchi kuacha uwindaji haramu, kutunza misitu ya asili, kuhakikisha kila kaya inapanda
miti isiyopungua 10 kila mwaka na kuwafichua wale wote wanaoanzisha moto kichaa katika
mazingira.
Aidha amesema
kuwa kila wilaya
iandae taarifa ya uzuiaji moto
kichaa hasa kipindi cha kiangazi kwani
uchomaji misitu unarudisha nyuma uhifadhi wa mazingira ambapo atakayebainika kufanya hivyo kulingana na kifungu cha
sheria ya misitu no 12 atatozwa
faini ya sh laki 3 na kanuni ya sheria
ya makosa ya jinai kifungu no 21 na 22
kitatoa adhabu ya kifungo cha miaka isiyopungua 14 kwa atakayekiuka taratibu hizo.
Naye Meya wa
Manispaa ya Iringa Bw Amani Mwamwindi
amekiri Mkoa wa Iringa kushika nafasi ya kwanza kitaifa katika usafi na kueleza vitu vilivyopelekea kushika nafasi
hiyo kuwa ni upandaji wa miti, maua, mpangilio mzuri wa nyumba za watu, vyuo,
shule pamoja na zahanati.
Ikiwa ni mara ya kwanza Mkoa
wa Iringa kushika nafasi hii ambayo miaka kadhaa imekua
ikishikiliwa na wilaya ya Moshi iliyopo Mkoani Kilimanjaro wakazi mbalimbali
Mkoani Iringa wameonyesha kuguswa na
suala hili pamoja na kupongeza
juhudi zilizofanywa mpaka kufikia hatua hii na kuahidi kuyatunza
mazingira na kuhakikisha yanakuwa katika hali ya usafi.
Wednesday, June 4, 2014
WALEMAVU WAASWA KUJISHUGHULISHA BAADALA YA KUWA TEGEMEZI
Katibu wa chama cha walemavu wa macho Wasioona katika manspaa ya iringa David mgimwa amewataka walemavu wenzake kutotegemea misaada kutoka kwa serikali bali
wajishughulishe kwa kile kidogo wanacho kipata.
Akizungumza katika kikao chao kilichofanyika katika ofisi
za walemavu wa macho mjini iringa bwana David Mgimwa ameeleza kuwa anaomba ushirikiano
na serikali kwaajili ya kuanzisha chanzo cha mapato endelevu kitakacho kuwa
kinasaidia walemavu kimaisha.
Wakati huohuo Bw mgimwa ameomba misaada kutoka kwa
mashirika mbalimbali pamoja na serikali ili kujenga kituo kikubwa cha kulelea
walemavu hao pamoja na kituo cha kutolea huduma ya elimu.
Aidha
Katibu huyo ameongeza
kwa kusema kuwa anawashauri
walemavu wote wenye uwezo kidogo kuacha kutegemea misaada kila wakati bali wajishughulishe na sekta mbalimbali za
kiuchumi kwa kile wanacho kipata kutoka serikalini na taasisi binafsi.
UONGOZI MPYA WA TFF CHINI YA RAIS MALINZI WAMUINUA MVERA KUWA MKURUGENZI WA WANACHAMA WA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI
ALIYEKUWA KATIBU WA CHAMA CHA SOKA MKOA WA IRINGA ELIUDI MVELLA WAMAHANJI AJIUZULU RASMI ,SASA NI MATAWI YA JUU....
Aliyekuwa katibu wa chama cha mpira wa miguu mkoa wa Iringa Eliud Mvella Wamahanji ambae amejiuzulu nafasi hiyo rasmi |
Wamahanji katikati akizungunza na wanahabari mkoa wa Iringa sababu za kujiuzulu kwake |
Wanahabari mkoa wa Iringa wakimsikiliza aliyekuwa katibu wa chama cha soka mkoa wa Iringa Eliud Mvela Wamahanji kulia alipotangaza kujiuzulu nafasi yake |
Wamahanji akiwashukuru wanahabari Iringa kwa ushirikiano wao mkubwa |
Subscribe to:
Posts (Atom)